Kesi ya washukiwa wanne wa shambulizi la kigaidi la Westgate lililofanyika nchini Kenya mwaka jana, imeanza rasmi nchini humo.
Taarifa zinazohusiana
Kenya
Washukiwa hao wanne wameshitakiwa kwa kusaidia magaidi waliofanya shambulizi hilo ambapo watu 67 waliuawa na wengine 200 kujeruhiwa.
Wamekanusha mashitaka.
Kundi la wapiganaji wa kiisilamu al-Shabab lilikiri kufanya shambulizi hilo.
Maafisa wakuu nchini Kenya wanaamini kuwa washambuliaji wote wanne walifariki wakiwa ndani ya jengo hilo.