Quantcast
Channel: MATUKIO NA VIJANA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 20290

WAZIRI MKUU PINDA AMEAGIZA MKURUGENZI NA MKUU WA WILAYA WANGING'OMBE KUHAMIA IGWACHANYA HARAKA.

$
0
0


 Askofu wa Jimbo la Njombe Alfred Maluma akieleza malengo ya Kuusaidia Mkoa wa Njombe.
 Mama Tunu Pinda naye apongeza Jitihada za Wakazi wa Wilaya ya Wanging'ombe.
 Mratibu wa Ujenzi wa Chuo cha Kilimo na Mifugo wilaya ya Wanging'ombe Padre Evodius Msigwa akisoma Taarifa ya Chuo Hicho kwa Waziri Mkuu.

na gablriel blog
 Mbunge wa Jimbo la Njombe Magharibi ambaye Pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Gerson 
Lwenge
 Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Bi.Esterina Kilasi akisoma taarifa ya Wilaya Hiyo kwa Waziri Mkuu Akiwa Katika Kijiji cha Ilembula.
 Waziri Mkuu Pinda akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Leo wakati wa Ziara yake ya Wiki Moja Mkoani Njombe.
 Waziri Mkuu akiweka Jiwe la Msingi Katika Ujenzi wa Bweni la Wasichana katika Shule ya Sekondari ya Igwachanya

 Chief wa Kabila la Wabena ambao ndio Wataalamu wa Kimila Mdandu na Msitu wa Nyumbanitu Mzee Mbeyela.
 Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Kilimo Mkoa wa Njombe NADO Bwana John Wihallah Akisoma taarifa ya Shirika Hilo Kwa Waziri Mkuu wakati alipotembelea na kukagua maonesho ya Wajasiliamali Igwachanya.
 Mbunge wa Viti Maalumu wa Vijana Bi.Msigwa

Hii Ni Bendera ya Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

Na Gabriel Kilamlya Wanging'ombe.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda Amewataka Wakuu wa Wilaya na 

Wakurugenzi wa Halmashauri Mkoani Njombe Kutafuta Namna ya 

Kupunguza Tatizo la Maji Linaloonekana Kuwa Sugu Mkoani Hapa.

Aidha Waziri Mkuu Amewataka Viongozi Hao Kutafuta Wafadhili 

Mbalimbali Watakaosaidia Kujenga Miradi Mbalimbali ya Maji Kama Vile 

ya Visima Ambayo Inaweza Kuanza Katika Hatua za Muda Mfupi za 

Kupunguza Tatizo Hilo.

Akizungumza Wakati wa Kuweka Jiwe la Msingi Katika Chuo Cha Kilimo 

na Mifugo Mayale Ikiwa ni Siku Yake ya Kwanza ya Ziara ya Wiki Moja 

Mkoani Njombe,Waziri Mkuu Mizengo Pinda Amesema Bila Maji ya 

Uhakika ni Vigumu Kupata Maendeleo ya Kilimo.

Aidha Amewataka Maafisa Ugani Kuhakikisha Wanawafikia Wakulima na 

Wafugaji Mashambani Badala ya Kuendelea Kukaa Ofisini Kwa Kisingizio 

Cha Ukosefu wa Usafiri.

Sanjali na Hayo lakini Pia Ameagiza Mkurugenzi Pamoja na Mkuu wa 

Wilaya ya Wanging'ombe Kuhamia Igwachanya Mwishoni Mwishoni mwa 

Mwezi Huu.

Awali Akisoma Taarifa ya Chuo Hicho Mratibu wa Chuo Hicho Mchungaji 

Evodeus Msigwa Amesema Chuo Hicho Kinajengwa Chini ya Ufadhili wa 

Nchi ya Italy na Lengo Hasa ni Kwaajili ya Kuwasaidia Watu Wenye 

Ulemavu na Vijana.

Ziara ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda Imeanza Leo Mkoani Njombe na 

Kutarajiwa Kudumu Kwa Wiki Moja Huku Akitarajiwa Kutembelea Maeneo 

Mbalimbali Mkoani Hapa

Viewing all articles
Browse latest Browse all 20290

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>