Hii ndio barabara kuu inayotoka Kilombero kuelekea lfaraka,Mahenge na Ulanga,eneo hili limekuwa kero kubwa kwa wasafiri wanaotumia barabra hiyo,
WANANACHI wanautumia barabara kuu ya kilombero,kuelekea maeneo ya lfaraka,Mahenge,na Ulanga,wameilalamikia serikali ya wilaya ya kilombero kwa kushindwa kukalabati shimo kubwa lililopo barabara kuu ya Kilombero-lfaraka na kusababsiha adhabu kubwa kwa wananchi ambao magari yao hukwama kwenye shimo hilo na kusababisha kulala hapo usiku kucha.
Shimo hilo klubwa lililojaa maji kufuatia mvua zinazoendela kunyesha lipo kwenye barabara hiyo eneo la Kidatu kilometa chache kitoka Kilombero mjini
Baadhi ya wananchi waliohojiwa na audifacejackson blog walidai kwamba shimo hilo ni la muda mrefu na kwamba viongozi mbali mbali wanapita eneo hilo na kushuhudia bila kuchukuha hatua yoyote.” Bila huyu jamaa mwenye trekta sijua hali ingekuaje,hata hivyo jamaa huyu anafanya kazi hii kwa muda wa mchana tu ikifika jioni anaondoka zake, jana usiku kuna abiria wa basi moja walipofika hapa wamekwama na dereva alifanya jitohadi kulivusha gari lake bila mafaniki nakuradhimika kulala hapa huku baadhi ya abiria waliokuwa na watoto wadogo wakilalamika watoto zao kung’atwa na Mbu na kupigwa na baridi usiku kucha hadi alfaji trekta lilipofika na kulivuta basi hilo, wananchi tutavumilia lakini iko siku uvumilivu utafika kikomo”alisema Bw Abdalaman Ismail ambaye alikuwepo eneo la tukio alishuhudia ndugu zake wakitaabika kwenye eneo hilo.
Trekta ambalo linafanya kazi ya kuyafuta magari yanayokwama kwenye shimo hilo,likifuta roli huku mataili yote manne yakiwa juu kufuatia roli hilo kuwa na mzigo mzito
Basi hili likijitoa kutumbukia kwenye shimo hilo
Wananachi wakieleke kwenye basi lao ambalo lilikwama eneo hilo kwa muda mrefu,na kufanikiwa kuvutwa na trekta hiyo