
''Kocha Brandts''
MWENYEKITI wa Yanga, Yusuph Manji ameitisha mkutano na wanahabari akitaka akuzungumzia pambano la jana dhidi ya Simba katika mchezo wa Nani Mtani Jembe huku kukiwa na taarifa kwamba kuna mambo mawili anayoweza kutoa maamuzi katika mkutano huo.
Moja ya linaloelezwa atalitangaza ni kumtimua kocha mkuu wa klabu hiyo Ernie Brandts au kubwaga manyanga kutokana na aibu aliyoipata jana uwanjani wakati Yanga ikilala kwa mabao 3-1 mbele ya Simba.
Credit: micharazomitupu.blogspot.com