Bingwa wa michezo ya all African Games mwaka 1973 ndg Kipchoge Keino (KULIA) wa Kenya ambaye ndiye mkimbizaji wa kifimbo cha malkia akiwa na mmliki wa blog ya Lenzi ya michezo |
Watoto wa shule ya Filbert Bayi wakicheza ngoma |
JKT Mgulani |
MJUMBE wa Baraza la Michezo ya Jumuiya ya Madola, Kipchoge Keino ameitaka serikali kuweka mipango dhabiti ya kuendeleza michezo.
Keino ambaye ndiye mkimbizaji wa kifimbo cha malkia aliyasema hayo wakati alipotua Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere na kupokele na viongozi wa serikali na kamati ya Olmpiki Tanzania.
“Tanzania ina vipaji na hili nalijua kwani nilikuwa na Filbert Bayi kwenye mashindano mbalimbali ya kimataifa hivyo mikakati ikiwekwa ya kuendeleza vipaji nchini itapata medali nyingi kwenye mashindano ya kimatifa”’ alisema Keino ambaye alishawahi kuwa bingwa wa mashindano ya Afrika (all African Games)
Kifimbo hicho kiliktua nchini kikitokea nchini Rwanda na kukabidhiwa kwa Rais wa Kamati ya Olympiki Tanzania Rashid Gulam na leo kitakimbizwa katika mitaa na barabara kadhaa za jijini la Dar es Salaam na Baadae kitapelekwa Ikulu kabla ya kwenda Zanzibar .
“Kifimbo cha Malkia kesho kitakuwa hospitali ya Muhimbili kwenye wodi ya watoto wenye ugonjwa wa saratani ili wacheze nacho, baadae kitapelekwa Uwanja wa Taifa ili watu wakione na kupiga picha, baadae kitakimbizwa katika barabara ya Nelson Mandela kikifika TAZARA kitapitia barabara ya Nyerere kurudi mjini kupitia Gerezani baadae kitapelekwa Ikulu ambako kitapokelewa na Rais Jakaya Kikwete:, alisema Jabir ambaye ni katibu wa kamati Maalum ya TOC”, alisema
“Kikiwa Zanzibar kitakimbizwa Mji Mkongwe na sehemu nyingine za Historian a baadae kitapelekwa Ikulu ya Zanzibar”, alisema
Pia Jabir aliwataka wakazi wa jiji la Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kukimbiza kifimbo hicho kwani watanzania wana historia ya kuwa wakarimu.