Zimbabwean Prime minister  Morgan Tsvangirai gestures during a press conference at Movement for Democratic Change party headquarters in Harare, Friday, October, 16, 2009. Zimbabwe's prime minister announced he was boycotting the country's troubled unity government Friday, citing the "persecution" of a top aide being tried in an alleged coup plot. (AP Photo/Tsvangirayi Mukwazhi)
Waziri Mkuu wa Zimbabwe Bw. Morgan Tsvangirai amesema muda uliobaki ni mfupi mno kuweza kutimiza siku iliowekwa kwa ajili ya uchaguzi wa kitaifa nchini humo.
Ameongeza kusema kuwa mabadiliko ya msingi ya kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na haki bado yanahitajika kutekelezwa.
Rais Robert Mugabe wiki iliyopita alisema atakubaliana na muda uliowekwa na mahakama ya katiba.

Uchaguzi huo utaashiria kumalizika kwa muungano ulioundwa na viongozi hao mwaka 2009 baada kura kuvurugiga.
Chama cha Movement for Democratic Change (MDC) cha Bw. Tsvangirai kiliungana na Zanu-PF cha rais Mugabe na kushirikiana kuunda serikali chini ya shinikizo la viongozi wa Afrika kwa nia ya kumaliza vurugu zilizodumu kwa muongo mmoja nchini Zimbabwe.